TENDI ( EPIC)




KALINJUMA DEZIDERY 2010-04-06330
 

NI KWA JINSI GANI TAFSIRI HUSAIDIA KUKUZA NA KUSAMBAZA FASIHI?



Makala hii ilikuwa moja ya kazi za utafiti wa kujisomea. Kazi hii iliandaliwa na kwa silishwa kwa wanafunzi kama kazi ya tendi za Kiswahili.

Utangulizi.

Makala hii inaelezea kuhusu tafsiri na nafasi yake katika kukuza na kusambaza fasihi, katika makala hii nitaanza kwa kueleza maana ya fasihi linganishi maana ya tafsiri kama ilivyofafanuliwa na wataalamu mbalimbali. Baada ya tafsili nitachambua tafsiri katika  fasihi linganishi  ya Kiswahili mkazo ukiwa zaidi katka mchango wake kama nyenzo muhimu katika kukuza fasihi. Pia makala hii itaonyesha utanzu ulioingiza kazi  za fasihi za kigeni kwa njia ya tafsiri,  utanzu unaokabiliwa na changamoto nyingi wakati wa kutafsiri na namna ya kukabiliana na changamoto hizo. Sehemu inayofuata ya makala hii itaonyesha kwa kina utanzu mmoja kati ya zilizopo kwenye jedwali kama kielelezo cha kueleza ubovu au  ubora wa kazi za fasihi na kisha utafuata uchambuzi wa kazi mojawapo ya fasihi msisitizo ukiwa hasa kwenye mchango wa tafsiri katika fasihi linganishi ya Kiswahili pamoja na changamoto zitokanazo na mchakato wa tafsiri katika kufasiri matini za kifasihi. Nikianza na maana ya fasihi linganishi na maana ya tafsiri kama zilivyoelezwa na wataalamu mbalimbali.

Wamitila (2003) anaeleza kuwa fasihi linganishi  inahusu uchambuzi wa maandishi ya wakati mmoja na aina moja na katika lugha mbalimbali kwa  nia ya kumiliki sifa zinazoyahusisha  kama athari, vyanzo, sifa zinazofanana na tofauti za kiutamaduni. Anaendelea kueleza kuwa inawezekana kufanya hivi kwa nia ya kuangalia matapo mbalimbali, maendeleo au hata nadharia za kiuhakiki. Fasihi ya namna hii iliweka misingi na juhudi za wanaisimu kuanza kuilinganisha lugha mbalimbali katika karne ya kumi na tisa. Hivyo tunaweza kusema kuwa faasihi linganishi inajikita zaidi kutumia mbinu za kiulinganishi  baina ya kazi mbili za kifasihi ili kujua sifa fulani fulani kama vile kufanana kwa kazi hizo, tafauti za kiutamaduni katika kazi hizo, kujua ulinganishi katika lugha yaani sarufi ya lugha katika kazi hizo za kifasihi.

Dhana ya tafsiri imejadiliwa na wataalamu wengi kama Mwansoko na wenzake (2006) Pia wakimnukuu Catford (1965),  Naye Newmark (1982) Nida na Taber (1969) waanaekea kufanana katika fasili zao kwani Newmark na Mwansoko wanasema kuwa ni zoezi la kuhawilisha ujumbe kutoka matini chanzi kwenda matini lengwa, wakati Catford anasema ni kuzalisha upya ujumbe

\
                                       
ulio katika matini chanzi katka matini lengwa na Nida na Taba wanasema ukuwa ni kuzalisha upya ujumbe wa lugha chanzi kwa kutmia visawe vya asili vya lugha lengwa vinavyo karibiana na lugha chanzi kimuundo na kimaana. Hivyo tunaweza kuona kuwa wataalamu hawa walicholenga ni kufikisha ujumbe wa matini cha nzi katika matini lengwa. Baada ya kuona fasili ufuatao ni umuhimu wa  tafsiri katka fasihi.
Tafsiri ni nyenzo muhimu katika kukuza na kusambaza fasihi. Tafsiri ndilo daraja linalo unganisha jamii za watu wanaotumia lugha zinazotofautiana. Katika kufanya hivi kuna uibukaji wa misamiati mipya ambayo hapo awali haikuwepo katika lugha Fulani G. Ruhumbika  katika Makala za semina ya kimataifa ya waandishi wa Kiswahili (ii) anaeleza kuwa maneno ya kigeni katika lugha nyingine ni ya msingi sana na tunaendelea kuyahitaji sana. Maneno haya yanakubalika na yanatumika mpaka sasa. Maneno katika lugha yanaweza kuingizwa ka kutoholewa, kukopwa, kuhawilishwa nkadhalika.
 Fasihi ya Kiswahili imeanza kuchapishwa nje ya chi na bara la afrika. Mwansoko na wenzake (2006) wanasema ‘shughuli za wazalendo zimejalizwa na mashirika ya ufasiri na uchapishaji ya nchi za nje ambayo yamefanya kazi kubwa ya kupanua hazina ya vitabu vya Kiswahili. Baadhi ya mashirika hayo ni shirika la uchapishaji lugha za kigeni, Beijing china, shirika la uchapishaji la maendeleo na shirika la uchapishaji la Ruduga yote ya Moscow, Russia, Longmans nk. Miongoni mwa tafsiri za Kiswahili za mashirika haya ni pamoja na shajara ya mwenda wazimu na hadithi teule za Lu Kun. Kutokana na maendeleo tafsiri fasihi ya Kiswahili imesambaa na kuwafikia watu wa mataifa mbalimbali.
Waandishi wengi wamejifunza mbinu za uandishi kutoka mataifa mengine. Mfano mtindo wa uandishi, ujenzi wa wahusika na ubunifu wa mandhari na mbinu nyingine za kisanaa. Hii imeifanya fasihi ya Kiswahili kukua na kuweza kufanyiwa ulinganisho na fasihi nyingine za kilimweengu mfano tamthiliya ya Amezidi ya Said A. Mohammed. Waandishi wengine kama Kezilahabi, Pamoja na wamitila. Waandishi hawa waliandika kazi zao sambamba na fasihi za kiulimwengu. Hivyo huenda ni kutokana na kusoma kazi nyingi za tafsiri wameweza kuibuka na
aina hii ya uandishi iliyo ikuza fasihi ya Kiswahili hadi kufikia ngazi moja na fasihi za kilimwengu.
MAPITIO YA KAZI ZA FASIHI ZILIZOTAFSIRIWA

JINA LA KAZI
UTANZU
  MFASIRI
MWAKA
TAFSIRI







1.
Barua ndefu kama hii.
Riwaya
C. Maganga
1994
Kifaransa-Kiswahili
2.
Wema hawajazaliwa
Riwaya
A.Abdallah
1996
Kiingereza-Kiswahili
3.
Alfa-lela ulela namba kitabu 2.
Hadithi fupi
Hassan Adam
2004
Kijerumani-kiswahili
4.
Alfa-lela ulela kitabu 4
Hadithi fupi
Edwin W. Brenn
1994
Kiingereza-Kiswahili
5.
Robinson crusoe
Hadithi fupi
Genesis Press Kiswahili
2010
Kiingereza-Kiswahili
6.
Wimbo wa lawino
Ushairi
P. Sozigwa
1975
Kiingereza-Kiswahili
7.
Sundita
Tamthiliya
E. mbogo
2011
Kiingereza-Kiswahili
8.
Aliyeonja pepo
Tamthiliya
Martin Mkombo
1980
Kiingereza-Kiswahili
9.
Nitaolewa nikipenda
Tamthiliya
C. Mkabugi
2010
Kiingereza-Kiswahili
10.
Orodha
Tamthiliya
S. D. Kiango
2006
Kiingereza-Kiswahili
11.
Mkaguzi muungwana
Tamthiliya
A.Morrison
1961
Kiingereza-Kiswahili
12.
Mnafiki
Tamthiliya
L.Taguaba
1973
Kiingereza-Kiswahili
13.
Mfalme edpode
Tamthiliya
S.S. Mushi
1971
Kiingereza-Kiswahili
14
Masaibu ya ndugu jero
Tamthiliya
A .S. Yahya 
1974
Kingereza- Kiswahili
15
Mkaguzi mkuu wa serikali
Tamthiliya
C. Mwakasaka
1979
Kingereza-kiswahili.
16
Mnafiki
Tamhiliya
L. Taguaba
1973
Kingereza-Kiswahil .

Kazi ya tafsiri ni nyenzo kubwa katika kueneza na kukuza fasihi kwani kutokana na kazi kutafsiriwa kutoka lugha mbalimbali huifanya lugha hiyo ikue kwa kuongeza msamiati na idadiya watumiaji.  Baada ya kuona umuhimu ifuatayo ni tathimini ya kazi ya tafsiri.
KALINJUMA DEZIDERY 2010-04-06330
Katika kutathmini mapitio ya kazi za tafsiri zilizotafsiriwa kutoka lugha mbalimbali, utanzu wa tamthiliya unaonekana kutafsiriwa zaidi na kuingiza kazi za kiafasihi nyingi za kigeni kuliko tanzu nyingine. Hii ni kwa sababu;
Hutafsiriwa ili isomwe na hutafsiriwa ili iweze kuigizwa jukwaani. Kutokana na mchezo wa uigizaji kuwa kichocheo kikuu cha kuburudisha jamii, tamthiliya imepata sifa ya kutasiriwa zaidi ili
iweze kuigizawa jukwaani. Pia kutokana na muundo wake wa majibizano ambao huleta hamu an kuvuta hisia wakati wa usomaji umefanya kuwepo na wahitaji wengi wa kusoma tamthilya hivyo kikawa chanzo cha kufasiriwa zaidi. Mifano iko katika jedwali.
Lugha zilizojitokeza katika kufanikisha suala la tafsiri ya Kiswahili ni kiswahili kwani kutokana na idadi ya tafsiri nilizokusanya, tafsiri nyingi zinaonekana kutafsiriwa kutoka kiingerza kwenda Kiswahili na nyingine chache zimetoka lugha ya Kikerewe, kijerumani, na kifaransa. Hii ni kutokana na data nilizo kusanya.
Utanzu uokabiliwa na changamoto zaidi wakati wa kutafsiri ni ushairi. Newmark (1988)anasema  ushairi ndiyo utanzu wa fasihi uliomgumu zaidi kutafsiri. Utanzu wa ushairi huwa mgumu kutokana na kuandikwa kisanii zaidi ili kulidhisha na kufurahisha nafsi ya mwandishi. Ushairi huzingatia zaidi vipengele vya fani. Jambo la kwanza la maana katika kutafsiri ushairi ni neno likifuatiwa na msitari. Tofauti na zilivyo tanzu nyingine za fasihi. Licha ya kubeba maana za kawaida neno katika ushairi aghlabu huwakilisha sauti na milio mbalimbali ambayo mfasiri lazima aioneshe pia katika matini lengwa ili ujumbe uliokusudiwa ufike.
Katika kutafsiri ushairi lazima kuzingatia vipengele vyote vya fani kama sitiali, tamathali za semi, ishara, tashibiha na vingine. Hivyo ni lazima kila neno na mstari katika ushairi vizingatiwe kwa uzito uleule kama ulio katika matini chanzi. Mfano kama sitiari au ishara, sauti zina visawe katika lugha chanzi basi vitafutiwe visawe katika lugha lengwa ili kutimiza uhalisia wa lugha chanzi.
Hivyo ni vigumu kufasiri ushairi kutokana na uteuzi wa lugha katika matini chanzi. Na ni vigumu sana kwa shairi lililo tafsiriwa kulingana na shairi chasili katika uzito wake. Ili kuepuka changamoto hizo lazima mfasiri ajue utamaduni wa lugha chanzi na lugha lengwa ili kuweza kufasiri kulingana na utamaduni wa jamii lengwa. Pia mfasiri anaweza kufasiri kulingana na jinsi shairi linavyomwingia au linavyomchoma na kumwathili yeye mwenyewe yaani mfasiri ajichukulie yeye ndiye mlengwa wa tafsiri anayoifanya.
Katika kubainisha ubora au udhaifu wa tafsiri nimeteua tamthiliya ya “Black hermit” kilichoandikwa na Ngugi wa Thiong’o (1968) na kutafsiriwa kama “Mtawa mweusi” na EAEP ltd (2008). “Black Hermit” Katka kuchambua kigezo hiki cha ubora na ubovu wa tafsiri nimegundua kuwa tafsiri ya “Mtawa mweusi” ni tafsiri bora kiasi kwani ameweza kuzingatia vpipengele vilivyo katika matini chanzi mfano ujumbe, miundo ya maneno, alamaza uandishi na nyingine. Lakini kuna makosa ambayo mfasiri huyafanya wakati wa tafsiri ambayo kiuhakika yanaweza kuiwekwa tamthiliya hii katika ubovu mafano: uongezaji wa maana, udondoshaji wa baadhi ya vipengele, kuacha baadhi ya maneno, uteuzi mbaya wa msamiati ambao hubadili lengo la matini chanzi, kubadili muundo wa matini chanzi na upotoshaji ambao hupoteza maana ya matini chanzi.
Kutokana na uchambuzi wa tamthiliya ya “Mtawa Mweusi” nimegundua kuwa tafsiri ina mchango mkubwa katika fasihi linganishi ya Kiswahili. Kwa kulejelea tafsiri ya Mtawa Mweusi tunaweza kugundua utamaduni wa jamii fulani mfano tunaona utamaduni wa jamii ya Marua ambayo imejaa mambo mengi ya kulinganisha na jamii nyingine. Mfano kurithi wajane, kukatazwa kuoa nje ya utamaduni nk.
Mfano; mara baada ya hapo baba yangu akawa mgonjwa alikuwa na mshutuko baada ya kifo cha kaka yangu! Aliniita kitandani kwake akaaniambia “Remi unafahamu desturi yetu mke wa kaka yako sasa ni mkeo”
Mfano huu unatudhirishia uwepo wa utamaduni wa kulithishana wamawake katika jamii ya Marua. Ikilinganishwa na jamii ya leo hii katika afrika bado utamaduni huo upo katika baadhi ya jamii.
Tafsiri pia inatujuvya kuhusu historia ya jamii fulani ambayo inaweza kulinganishwa na jamii nyingine katika vipindi mbalimbali vya mapitio katika kuelekea maendeleo. Jamii ya marua imepitia vipengele tofauti tofauti vya maendeleo vivyojaa misuko suko ya kukataliwa kusikilizwa maoni yao, kunyanyaswa, kusalitiwa na kuvymwa haki yao. Mfano;
Lakini kwanini kumnyang’anya mfanya kazi chombao hicho kimoja atumiacho? Chama chochote cha wafanyakazi bila kugoma ni mfano wa samba asiye na makucha wala meno
Umuhimu mwingine wa tafsiri katika fasihi linganishi ni pamoja na kutujuvya kuhusu itikadi ya jamii Fulani. Katika yafsiri hii nimeweza kugundua itikadi za aina mbili, itikadi ya kaifrika juu ya wazungu na itikadi ya wazungu juu ya waafrika. Hii inawakilishwa na jamii ya marua ambayo haiwezi kuoa nje na kabila lake hasa mzungu. Hii wanaihusisha na athari waliyopata wakati wa ukoloni. Mfano Remi anakataa kumuoa Jane kwa sababu ya tofauti ya kabila na itikadi. Mfano.
Remi: “Wewe ni tofauti na mimi, na sisi, na kabila. Huwezi kufahamu yale ninayo fahamu. Oh nafahamu baba yako hakuwa mlowezi, alikuwa mwalimu mmoja wa wawatu wema…”
“Tunawezaje kuwa sawa? Wito wa kabila unawezaje kuwa wito wako”?.
Maelezo haya kiujumla yanaonesha kuwa kabila la marua hawakuwa tiyari kuwaoa watu walio nje ya kabila lao mfano wazungu. Kuhusu itikadi ya wazungu, wao hawaoni haja ya kutengana kutokana kwasababu ya rangi za ngozi zao au  kabila bali wao wanasisitiza uelewano tu akti ya mtu na mtu.
Mfano:           Jane
“Maana watu wote ni wamoja kila mahali. Hoja siyo utaifa, imani wala mila bali kama watu wanaweza kuelewana   wao kwa wao.”
 Kuligana na maelezo haya, yakilinganishwa  na hali ya kawaida katika kabila mabalimbali hayatofautiani kwani ni jamii nyingi za kiafrika itikadi zake  zinatofautiana na za wazungu.
Pamoja na tafsiri inayofanyika, kuna changamoto zinazotokana na mchakato wa tafsiri. Chanagamoto hizo zinatokana na hoja moja kuu sana ambayo I ukosefu wa ujuzi juu ya lugha inayotumika katika tafsiri lengwa. Mfano wafasiri wa lugha ya Kiswahili hukosa umahili walugha ya lugha lengwa. Tatizo hili ndilo chanzao cha kiila changamoto katika tafsiri. Changamoto zitokanazo na kukosa ujuzi wa lugha ni pamoja na; uteuzi mbaya wa msamiati, kushindwa vipengele vya  kisarufi, kuongeza maana isiyohitajika, kupunguza vipengele vya msingi katka matini chanzi, kuacha bila kufasiri baadhi ya vipele.
Changamoto nyingine ni pamoja na tofauti kitamaduni, tofauti za kimazingira, tatizo la kiisimu, itikadi tofauti,
Kwa kuitimisha naweza kusema kuwa tafsiri ni kipengele muhimu katka kujua na kujifunza mambo mengi kutoka katika jamii tofauti.


Marejeo
East African Educational Publishers Ltd (2008) Mtawa Mweusi. Kenya: Sitima Printers  
                          Stationers Ltd
Mwansoko, H.J.M. na wenzake (2006) Kitangulizi cha Tafsiri: Nadharia nMbinu.
                    Dar es Salaam: TUKI.
Newmark, P. (1982) Approaches to Translation. Oxford: Pergamon.
Newmark, P. (1988) A Textbook of Translaton. London: Prentice Hall.
 Ngugi wa Thing’o (1968) Black Hermit. Kampala-Uganda: East African Educational                             
                           Publishers Stationers Ltd
Nida, A. E. na Charles, R. T. (1969) The Theory and Practice of Translation. Netherlands:
                     EJ. Brill.
Ruhumbika, G. (1978) “Tafsiri za Kigeni katika Ukuzaji wa Fasihi ya Kiswahili” Makala
                    kwenye Semina za Kimataifa ya Waandishi wa Kiswahili Dar es Salaam.
Mohammed S.A. (2003) Amezidi. Nairobi : East African Educational Publishers.
Wamitila, K. W. (2003) Kamusi ya Fasihi: Istilahi na Nadharia. Nairobi: Focus Publication


                   TENDI ZA KISWAHILI. 
 



CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
TAASISI YA TAALUMA ZA KISWAHILI

   
                  TASWIRA YA KIFO CHA SHUJAA KATIKA UTENDI:  SHUJAA                                    LIYONGO NA EMANUEL (YESU) KATIKA BIBLIA


                                                      
                                                       YALIYOMO

SEHEMU YAKWANZA.. 2
Utangulizi 2

SEHEMU YA PILI. 3
HISTORI YA SHUJAA FUMO LIYONGO NA EMANUEL.. 3
1.1       Historia ya Shujaa Fumo Liyongo. 3
1.2       Historia ya Shujaa Emanuel 4

SEHEMU YA TATU.. 5
Taswira ya Kifo cha shujaa Liyongo na Emanuel katika Biblia. 5

SEHEMU YA NNE.. 9
A.  Kufanana na kutofautiana kwa shujaa Liyongo na  Emanuel 9
1.Kufanana. 9
2.Kutofautiana Kwao. 9
B.    Hitimisho. 10

C.   MAREJEO  1


SEHEMU YAKWANZA

TENDI  NI NINI? 

Tenzi  za  Kiswahili zimepata mjadala mkubwa hasa katika vipengele  anuai  ambavyo  kwa  hakika  ndivyo   vinazibainisha  tenzi  za  Kiswahili  na hata  kuzitofautisha  na tenzi  nyingine zisizo  za Kiswahili. Miongoni  mwa  mambo  ambayo  yamepata mjadala  ni upatikanaji  wa  historia  katika  tenzi  za  Kiswahili. Mjadala  huu  umekitwa  katika  maswali  mbalimbali kama  vile, tenzi za Kiswahili  zinahusu nini? Kuna uwezekano wa kupata  historia  katika  tenzi  za  Kiswahili? Historia zinazopatikana  katika  tenzi  za Kiswahili zina ukweli na uhalisia  wowote? Historia  katika  tenzi za  Kiswahili  inatokana na  ngano  au  visasili? Ukweli  huo  ni wa  kisanaa  au  kijamii? Na ni kwa  namna gani  watunzi  wa tenzi  wanapata  historia  za  Waswahili? Makala  haya  yamelenga  kujadili  upatikanaji  wa  historia katika  tenzi  za  Kiswahili  na  ukweli  halisi  wa  kihistoria katika jamii  za  Waswahili.

1.0  UTANGULIZI
TENZI  ZA  KISWAHILI
 Dhana  ya  tenzi  imetazamwa  kwa  mitazamo  tofauti  ambayo  wakati  mwingine  hutofautiana. Ufasili  wa  tenzi  umekuwa ukielezwa  kwa kuangalia  sifa.  Katika  makala  haya istilahi  itakayotumika ni tenzi ambayo  itakuwa  na maana  sawa  na tendi  hivyo istilahi   zote zinatumika sawa. Wataalamu  mbalimbali  wamejaribu  kufasili  dhana  ya tenzi / tendi kama  ifuatavyo.
 Casco (2007) anaeleza kuwa utenzi  umetokana na  kitenzi tenda ambacho  kina maanisha  kufanya  tendo. Anabainisha  kuwa  utenzi  huwa na mistari  minne  yenye  silabi  nane kwa  kila  kipande,  mistari  huwa  na muungano  wa matukio, unaweza kuhusu  falsafa  au  masuala   ya  kidini, unaweza  kutoa  simulio  ya kweli au ya kubuni  na  huwa  na utangulizi, kiini na   hitimisho. Mtaalamu  huyu  anaeleza  kuwa  kuna  ugumu  katika  kutafuta  kisawe  mwafaka  cha utenzi katika  lugha  mbalimbali. Baadhi  wanasema  wimbo, ushairi  na  ushairi  mrefu.
Kutokana  na fasili  ya  Casco  tunapata  wazo kuwa  utenzi  huwa  na  matendo  katika  utendaji wake. Matendo  hayo hujidhihirisha  unapokuwa  katika  masimulizi,  kwa maana  hiyo  utenzi  ulio katika  maandishi hupoteza baadhi  ya  vionjo  vya kiutendaji.

 Wamitila (2003) amejadili  utendi  kama shairi refu la kisimulizi  linalozungumzia kwa  mapana  na mtindo  wa  hali  ya  juu  matendo  ya mashujaa  au  shujaa  mmoja. Anasema kuwa  utendi  huwa  na  sifa nyingi  na  huweza  kuleta  pamoja  hadithi  ya  shujaa, magari, visasili, historia, pamoja  na  ndoto  za  taifa  fulani.
Fasili  hii inatupa  utata  inapoeleza  utendi  kama  shairi  refu  la  kisimulizi. Utata  unajitokeza  katika  kupima  urefu  wa  ushairi  ulio  katika  masimulizi. Tutatumia  kipimo  gani  kupima  urefu  huo? Na mpaka wa  ushairi  mrefu na mfupi unaanzia wapi na  kuishia wapi. Fasili  hiyo inahitaji maelezo zaidi ya kipimo kipi  kinafaa  kutumika. 

Mulokozi (1996) anaeleza  utendi  ni ushairi  wa  matendo. Ni utungo  mrefu  wenye  kusimulia  matukio  ya  kishujaa  yenye  uzito  wa  kijamii  au  kitaifa. Matukio  hayo  yanaweza  kuwa  ya  kihistoria  na  visakale.
Ufafanuzi  huu  wa  Mulokozi  umepiga  hatua  mbele  kwa kueleza  utendi  kama  ushairi  wa  matendo. Utendi  hufungamana  na matendo  wakati wa utendaji  wake. Matendo  hayo huathirika utendi  unapokuwa katika maandishi.

  Kutokana  na  fasili  za  wataalamu  hawa  tunaweza kusema  kuwa  utendi  ni  ushairi  unaosimulia  tukio  fulani  kwa  matendo. Usimuliaji  wa  tukio  huambatana  na  matendo ambayo hufanywa  na msimuliaji. Utendi  unaweza  kuhusu  tukio  lolote  la  kijamii ambalo  laweza  kuwa  la kishujaa  au  lisiwe  la  kishujaa.

Makala hii imekusudia kufafanua taswira ya kifo cha shujaa katika utendi kwa kurejelea kifo cha shujaa Liyongo kama alivyoelezwa katika kitabu cha Tenzi Tatu za Kale kilichohaririwa na Mulokozi mwaka (1999) na shujaa Emanuel (Yesu Kristo) kama anavyoelezwa katika Biblia takatifu.

Kabla ya kujikita katika ufafanuzi huo ni muhimu kufahamu dhana ya kifo, taswira, shujaa na utendi. Kwa kuanza na dhana ya utendi, Mulokozi (1996) anaeleza kuwa, utendi ni hadithi ya kishairi kuhusu mashujaa wa kihistoria na wa kubuni, wa jamii au taifa.  Anaendelea kueleza kuwa baadhi ya tendi  zina sifa za kiriwaya, ila tu badala ya kuwa katika umbo la nathari zina umbo la kishairi.

Vile vile Mulokozi (1999) anarekebisha kidogo fasili yake na kueleza kuwa utendi ni utungo mrefu wa  kishairi wenye kusimulia hadithi ya ushujaa na mashujaa. Ukizichunguza fasili hizi utagundua kuwa tendi zina sifa ya kishairi, zinatokana na  masimulizi (zilizo nyingi), zinahusu mashujaa ambao wanaweza kuwa wa kihistoria au wa kubuni.  Pamoja na sifa hizo tendi pia huhusu masuala  mengine ya kijamii kama vile kutoa mawaidha kwa jamii, hivyo si lazima utendi umhusu shujaa peke yake.

Dhana ya kifo inaweza kufasiliwa kuwa ni kitendo cha kutolewa uhai au kupatwa na mauti kama ambavyo Mohamed (2002) ameeleza kuwa kisawe cha kifo ni mauti au ufu. Vile vile Wamitila (2003) amefafanua dhana ya taswira kuwa hutumiwa kuelezea neno, kirai au maelezo ambayo yanaunda picha fulani katika akili ya msomaji. Anaendelea kueleza kuwa, taswira zinaweza kuwa za kimaelezo ... (yaani maelezo fulani yaliunda picha) au za ki-ishara (zinazounda picha ambayo inaashiria jambo fulani au imeficha ujumbe mwingine).

Kwa mujibu wa Wamitila (2003) neno shujaa, hutumika kuelezea mhusika mkuu katika kazi ya kifasihi ambaye anaweza kuwa wa kike au wa kiume.  Kimsingi neno hili haliashirii wema tu.

Mulokozi (1996) kwa upande mwingine ameeleza kuwa, mashujaa wa utendi wa Kiswahili ni wa aina tatu (3) ambazo ni mashujaa wa kijadi wa Kiafrika, kwa mfano  Fumo Liyongo katika  Utendi wa Fumo Liyongo (Mohamed Kijumwa K 1913) na Abushiri bin Salim katika Utendi wa Vita vya  Wadachi Kutamalaki Mrima (Hemed Abdallah K, 1895), mashujaa wa kidini, hasa  mtume Muhamadi na masahaba wake (k.m. utendi wa Ras ‘lghuli) na  mashujaa wa kubuni  kwa mfano Tajiri katika Utendi wa Masahibu.

Mulokozi anaendelea kueleza kuwa, kati ya aina hizo tatu za mashujaa, riwaya  ya Kiswahili  imetumia mbili tu.  Wahusika wa  kijadi wa Kiafrika na wahusika wa kubuni.  Wahusika wa kidini hawajatumiwa kikamilifu (uk. 42) Kutokana na ufafanuzi huu ni dhahiri kuwa, mashujaa wa kidini bado hawajaelezwa ipasavyo na ndio sababu makala hii imejikita katika kuelezea angalau kwa sehemu kuhusu shujaa Emanuel katika Biblia akihusishwa na shujaa wa kihistoria na wa kijadi   Fumo Liyongo  katika Utendi wa Fumo Liyongo.

Baada ya kufahamu utangulizi huu, sehemu inayofuata itahusu historia  ya mashujaa waliokwisha tajwa hapo juu.

SEHEMU YA PILI

HISTORIA YA SHUJAA FUMO LIYONGO NA EMANUEL


1.1       Historia ya Shujaa Fumo Liyongo

Fumo Liyongo ni shujaa kama alivyoelezwa na Muhamadi Kijunwa mwaka 1913 katika Utendi wa Fumo Liyongo.  Mwandishi amesimulia habari za shujaa huyu kwa njia ya maandishi katika umbo la kishairi.  Japo kuna utata kuhusu tarehe aliyozaliwa Liyongo lakini tarehe inayoelekea kukubaliwa zaidi ni ile ya karne ya 13 – 14 kwa kuwa kitabu cha Terehe ya Pate (Freeman-Grenville 19962: 241 – 299) kinamtaja mtawala wa eneo la Ozi aitwaye Fumo Liyongo aliyeishi wakati wa utawala wa Fumomari (Fumo Omari), mtawala wa ki-Nabhany wa dola ya Pate.  Fumomari alitawala miaka ya 740 – 795 Hijriya (Miaka ya Kiislamu), sawa na 1340 – 1393 M. Liyongo huyo alipigana na Fumomari (Mulokozi 1999).

Mwandishi huyu anaendelea kutujuza kuwa vyanzo vinaonesha kuwa Liyongo aliishi  Pwani ya Kaskazini mwa Kenya kwenye maeneo ya Pate na Ozi kwenye karne ya 14 au kabla.  Mama yake aliitwa Samoa mwana.  Liyongo alikuwa kiongozi  katika jamii  yake, japo hakuna uhakika kama alikuwa mfalme.  Alikuwa shujaa, manju wa ngoma na malenga, na mwindaji hodari.  Kwa  upande wa dini, hakuna uhakika kama alikuwa ana Mkristo au Mwislamu japo  nyimbo zake zinaonesha kuwa huenda alikuwa mfuasi  wa dini ya Jadi ya Waswahili. Liyongo alikuwa akiwinda na kufanya biashara sehemu za bara karibu na Pate, aliweka makazi  yake Ozi, na  alifia na kuzikwa  Kipini, mahali paitwapo Ungwana wa Mashaha (Mulokozi na Sengo 1995:52-53). Ubeti wa 230 unaeleza kwa muhtasari maisha ya shujaa Fumo Liyongo

1.2       Historia ya Shujaa Emanuel

Emanuel ni shujaa wa kidini ambaye anaelezwa katika maandiko matakatifu yaani Biblia.  Kuzaliwa kwa shujaa huyu  kulitabiriwa na nabii Isaya (Isaya 9:6) sura ya 9 kifungu / mstari wa 6.
Tangu utabiri wa Isaya hadi  kuzaliwa kwake inakadiriwa kuwa ni miaka  400 k.k.  Utabiri wa nabii  Isaya ulitimia katika kitabu cha Mathayo 2:1 ambapo inaeleza kuwa shujaa alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi zamani za Mfalme Herode.  Kama ilivyo desturi ya mashujaa wengi wa kidini ,  baada tu ya kuzaliwa alikutana na vikwazo vya kutaka kuuawa na Mfalme Herode ambaye alihofia kunyang’anywa madaraka,  shujaa huyu atakapokuwa mkubwa (Math 2:13).  Malaika wa Bwana alimtokea Yusufu (Baba wa Emanuel) katika ndoto kumweleza kuwa amchukue mtoto Emanuel na mama yake (Mariam) kisha wakimbilie Misri.  Ndivyo ilivyo hata kwa mashujaa wengine, misukosuko inapozidi  kukimbilia uhamishoni.  Baada ya Mfalme Herode kufa shujaa Emanuel alirudishwa na wazazi wake Galilaya katika mji wa Nazareti.

Shujaa  Emanuel alibatizwa na Yohana katika mto Yordani.  Baada ya kubatizwa Roho wa Mungu alishuka juu yake kisha sauti ilisikika kutoka mbinguni ikisema “Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye”  (Math 3:13 – 17).  Shujaa huyu alibatizwa akiwa mtu mzima yapata miaka 27.  Baada ya kubatizwa alipelekwa na Roho Mtakatifu nyikani ili ajaribiwe na ibilisi, alifunga siku arobaini, mchana na usiku, kisha alishinda majaribu yote ya Ibilisi (Shetani)  (Math. 4:1 – 11).

Baada ya shujaa Emanuel kutoka nyika ni alichagua wanafunzi (wafuasi) kumi na mbili (12) ambao alikuwa anafanya nao kazi, na ndipo alipoanza huduma ya kuihubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna kwa watu (Math 4:17 – 25) akiwa   na miaka 27.  Baadhi ya  wanafunzi, wake ni Simoni Petro, Andrea, Yohana. n.k. Habari za shujaa huyu ilienea kutoka Galilaya, Dehapoli, Yerusalemu, Uyahudi na ng’ambo ya Yordani. Shujaa Emanuel alifanya huduma kwa muda wa miaka mitatu kisha akafa.  Wakati wa huduma ya kuwakomboa watu  na dhambi zao, wapo waliomkubali na kumfuata na wengine walimchukia na kumshutumu kuwa alikufuru kwa kujiita mwana wa Mungu. Wale waliomchukia ndio waliofanya njama za kumuua.  Hatimaye walimtumia mmoja wa wanafunzi wake aliyeitwa Yuda kwa kumpa vipande 30 (thelathini) vya fedha ili amsaliti kisha wamkamate.  Yuda aliwaambia, nitakayembusu ndiye, na hapo ndipo Wayahudi walipomkamata shujaa huyu na kumsulubisha hadi kifo chake (Marko 14:10-72 na 15:1-37).

SEHEMU YA TATU

Taswira ya Kifo cha shujaa Liyongo na Emanuel katika Biblia


1.         Taswira ya Kifo cha shujaa Liyongo
Liyongo ni shujaa aliyependwa na watu kwa kuwa aliwapigania na kuwasaidia, mfano aliwasaidia Waggala kupata mbegu bora (ub 40 – 41), aliishi porini na Watwa na kushirikiana nao vizuri,  ushirikiano uliomsaidia kumnusuru na njama za mfalme za kutaka  kumuua.

Kutokana na uhusiano mzuri aliokuwa nao na jamii yake Mfalme anamwonea wivu na anaogopa kuwa anaweza kumpokonya madaraka (ufalme). Anafanya njama za kumuua.  Njama  hizo hazifanikiwi na inabidi  mfalme amtumie  mwanawe Liyongo ili amsaliti baba yake kwa kuahidiwa kuozwa binti mfalme, kupewa uwaziri na mali nyingi.  Mtoto wa Liyongo anamuuliza babaye siri ya nguvu zake, anapoambiwa kuwa ni  kuchomwa sindano ya shaba kitovuni, anakubali kumchoma baba yake hatimaye Liyongo anakufa, kisha mwanawe  naye anakufa kutokana na uovu wake.

Baada ya shujaa Liyongo kufa watu walisikitika,  waliomboleza na wengine walionekana kukata tamaa kwa kuwa shujaa huyu alikuwa ni mtetezi wa watu katika jamii.  Beti za 224 – 226 zinaeleza vizuri jinsi watu walivyomwombolezea shujaa wao.

Taswira ya kifo cha shujaa Liyongo inaweza kujitokeza kwa namna tatu (3).  Kwanza kifo cha shujaa  Liyongo kwa mfalme ni mafanikio kwa kuwa ana uhakika wa kuendelea kutawala maana alikuwa na hofu kuwa Fumo Liyongo atamnyang’anya ufalme kwa vile alivyokuwa na mshikamano  na watu.  Pili, kifo cha Liyongo kwa mwanawe ni  adhabu kwani baada ya shujaa huyu kufa mwanawe naye alikufa kutokana na maradhi yasiyopona (ubeti 223) pamoja na kuchukiwa na  jamii yote kwa ujumla. (beti za 217 – 222).  Tatu kifo cha Liyongo kwa jamii yake ni sawa na kupoteza kitu chenye thamani kwa vile Liyongo alikuwa na  mshikamano na jamii yake. Baada ya kifo chake watu wanaomboleza na wanaonekana kukosa matumaini, haya yanayojitokeza katika (beti za 224 – 227).
Kwa upande wa fasihi, kifo cha shujaa Liyongo kimejengwa katika dhana ya usaliti unaosababishwa na tamaa ya madaraka (Ufalme) na tamaa ya mali (Mtoto wa Liyongo).  Mfalme (sultani) wa Pate anafanya fitina (Ubeti 49) za kumuua Liyongo akiogopa kupokonywa ufalme (ub. 93). Mwanawe Liyongo naye alikubali kumsaliti  baba yake kwa matarajio ya kuozwa mke (binti  wa mfalme), kupewa mali na uwaziri pia.  Dhana ya usaliti imejitokeza sana katika kazi  za kifasihi na inaonekana kuwa ni silaha ya kumwangusha shujaa mfano Lwanda Magere katika kitabu cha Lwanda Magere, Samsoni na Yesu katika Biblia.  Kwa upande mwingine dhana hii ina sura mbili yaani faida (anayenufaika baada ya usaliti) na hasara (anayeathirika baada ya usaliti).

Kifo cha shujaa pamoja na usaliti vinatupatia motifu ya dhambi na mapatilizi. Ingawa mtoto wa Liongo alimsaliti babaye ili apewe zawadi nono hakutimiziwa ahadi hizo. Alinyanyaswa na hatimaye alikufa kama alivyokufa baba yake. Hii inaashiria kuwa katika mapigano kati ya wema na uovu, siku zote wema hushinda. Kwa hiyo hata sultani hana maisha marefu. Historia imelishuhudia hili kwa kuwa muda si mrefu uatawala wa kisultani ulivamiwa na ukoloni, hata huo ukoloni nao leo hii haupo. Maisha ya milele ni maisha ya kutenda wena na haki.

2.         Taswira ya Kifo cha Shujaa Emanuel katika Biblia
Shujaa Emanuel alitabiriwa kuwa atazaliwa, atakufa na siku ya tatu atafufuka na kupaa mbinguni.  Jina Emanuel lina maana ya Mungu pamoja nasi.  (Math 1:22-23) maneno “Mungu pamoja nasi” yanarejesha uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu ambao  ulipotea katika bustani ya Edeni baada ya Adamu na hawa kutenda dhambi.  Baada ya anguko (dhambi) la Adamu na hawa, Mungu aliwaacha wanadamu kwa kuwa yeye ni mtakatifu na  hashirikiani (hashikamani) na uchafu (Mwanzo 3:1 – 24).

Kwa kuwa mwanadamu ameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu (Mwanzo 1:26 – 27), Mungu aliwahurumia na kuamua kuwaokoa tena kutoka katika utumwa wa dhambi na matendo ambayo shetani alikuwa akiwafanyia baada ya lile anguko la bustani ya Edeni.  Kwa sababu hiyo aliamua kumtoa mwanawe wa  pekee Yesu Kristo (Emanuel) afe msalabani ili awakomboe wanadamu.  Hivyo, kila atakayemwamini  shujaa Emanuel (Yesu Kristo) ataokolewa atoke katika utumwa huo wa dhambi na mateso yote ya Ibilisi na ndipo atakuwa ameunganishwa na Mungu yaani uhusiano wake na Mungu utarejeshwa tena yaani Mungu atakuwa pamoja naye.

Kifo cha shujaa Emanuel, japo kilitabiriwa kwa kuwa Mungu aliamua kuwarudia tena wanadamu lakini Yuda Iskariote ndiye  aliyepelekea kifo hiki kutokea.  Alimsaliti Emanuel kwa Wayahudi kwa tamaa ya pesa ya vipande thelathini (30).  Kama ilivyokuwa kwa shujaa Liyongo, Emanuel naye alisalitiwa na mtu wa karibu. (Mwanafunzi wake) kama Waswahili wasemavyo “Kikulacho ki nguoni mwako” (Luka 22:47). Habari za kifo cha shujaa huyu zimeelewa vizuri katika vitabu hivi:  Mathayo sura ya 26-27, Marko sura ya 14 – 15, Luka sura ya 22 – 23 na Yohana sura ya 13 – 19.  Yuda aliyewasaliti Yesu, baada ya kupewa vipande 30 vya fedha alimbusu Yesu, na Wayahudi, Waandishi na Mafarisayo wakamkamata na  kumtesa hadi alipokufa.

Taswira ya kifo cha shujaa Emanuel  kinajitokeza kwa namna mbalimbali kama ifuatavyo:  Kwanza Wayahudi, Waandishi na  Mafarisayo waliona kama wamemkomoa kwa kuwa walidai kuwa anajikweza kwa kujifanya mwana wa Mungu. Pia watawala walifurahi maana watu wengi walimfuata na kumsikiliza.

Pili, kifo cha Emanuel kilipoteza matumaini ya watu waliokuwa wakimwamini, ndugu zake (k.v. wazazi) pamoja  na wanafunzi wake.  Watu walilia na kuomboleza pale msalabani kwa kuwa mtetezi wao ametoweka japokuwa waliahidiwa kuwa siku ya tatu atafufuka.

Tatu, kifo cha Emanuel kwa Mungu kilikuwa ni kutimiza kusudi lake la kuwakomboa wanadamu, kwa kuwa alifanyika sadaka ya dhambi yaani alijitoa kafara ili wanadamu wasife tena kwa dhambi.

Nne, katika muktadha wa kifasihi tunaona nguvu ya usaliti katika kumwangusha shujaa.  Usaliti umeonekana  ukifanya kazi au kulisababisha shujaa kuanguka.  Hata katika maisha ya kawaida ya kila siku dhana hii inatenda kazi kwani tunashuhudia watu wakijiua kwa kuwa wamesalitiwa na wapenzi wao, ndugu au marafiki zao.

Kwa ujumla suala la usaliti limesawiriwa vizuri katika kazi mbili za Utendi wa Fumo Liyongo na Biblia.  Waandishi wamejitahidi kuonesha dhana hii kwa kuwatumia wahusika Liyongo na Emanuel.  Kwa mtazamo wangu, baada ya kuwachambua mashujaa hawa naona kuwa usaliti ni kipimo kinachotumika kupima nguvu aliyonayo shujaa, na nguvu inapobainika na watu wengine ndipo anguko la shujaa hutokea.  Mara nyingi anguko la shujaa husababishwa na watu wake wa karibu.


SEHEMU YA NNE

A.  Kufanana na kutofautiana kwa shujaa Liyongo na  Emanuel

1.         Kufanana

Mashujaa hawa wanafanana katika mambo yafuatayo
(i)                 Wote wanatumia  nguvu isiyokuwa ya kawaida kutenda mambo ya ajabu (miujiza).
(ii)               Walikuwa na ushirikiano mzuri na jamii zao.
(iii)             Walipendwa na watu kiasi cha watawala kuwachukia
(iv)             Walifanyiwa njama za kuuawa
(v)               Wote walisalitiwa na watu wao wa karibu
(vi)             Baada ya kufa watu waliwaombolezea.
(vii)           Wasaliti wa mashujaa wanaahidiwa kupewa fedha, vyeo na mali nyingine baada ya kukamilisha kazi ya usaliti mfano Mfalme  anaahidi kuwapa Wasanye, Wadahalo, Waboni na Watwa reale mia iwapo watamleta kichwa cha Liyongo.  Pia mwanae Liyongo anaahidiwa mali, mke na cheo cha uwaziri.  Pia Yuda aliahidiwa  vipande thelathini vya fedha iwapo atafanikisha kukamatwa kwa shujaa Emanuel.
(viii)         Waliowasaliti mashujaa Liyongo na Emanuel walikufa baada ya kifo cha mashujaa hao
(ix)             Hawakuwa waoga, wote ni majasiri.

2.         Kutofautiana Kwao

Shujaa Fumo Liyongo
Shujaa Emanuel
(i)
Fumo Liyongo alitumia nguvu ya uganga au sihiri. Hadhuriki  kwa chochote isipokuwa kwa kudungwa sindano ya shaba kitovuni.  (ubeti 143 – 144)
(i)
Alitumia nguvu za Roho Mtakatifu kutenda mambo mbalimbali k.v. kutembea juu ya maji, kuponya watu wengine (Mathayo 3:13-17, Mathayo 4: 23 – 25).
(ii)
Alioa mke na alikuwa na mtoto wa kiume, ana nguvu za kirijali
(ii)
Hakuoa wala hakuzaa
(iii)
Baada ya kufa hakufufuka
(iii)
Alifufuka na aliwatokea watu mbalimbali ili kuwadhihirishia kwamba yuko hai (Marko 16:1-14)
(iv)
Hakupaa kwenda mbinguni
(iv)
Alipaa kwenda mbinguni kuketi mkono wa kiume wa Mungu.
(v)
Hakufanikiwa kuikomboa jamii yake kwa kuwa alikufa
(v)
Japo alikufa kazi ya kuwakomboa wanadamu ilikamilika kwa kuwa kila atakayemwamini ataokolewa na kupatanisha na Mungu.

B.        Hitimisho

Katika kuhitimisha uchambuzi wa makala hii imebainika kuwa kila shujaa kati ya  hao wawili  alikuwa na wajibu fulani katika jamii yake ambao ilibidi autimize.  Katika kutimiza wajibu  huo shujaa lazima akutane na vikwazo ambavyo inabidi apambane na ashinde ili alete ukombozi kwa jamii yake.  Katika kupambana huko, wapo watakaomuunga mkono na wengine  kumpinga.Wale wanaompinga ndio hufanya njama za kumwangusha, wakifanikiwa shujaa hushindwa na wasipofanikiwa ndipo shujaa huyo hushinda na hivyo huleta mabadiliko katika jamii yake.

C.        MAREJEO


Bible Societies of Tanzania  and Kenya (1997).  Biblia: Maandiko Matakatifu ya Mungu.  The Bible Societies of Kenya and Tanzania: Nairobi  na Dodoma (Mtawalia)
Graf, H. (1980).  The Panarama Bible Study Coarse No. 1: The Plan of the Ages (Toleo la 1  la Kijerumani – Kiswahili. Kanisa la Biblia Publishers: Dodoma.
Mohamed, M.A. na Saidi, A.M (2002). Kamusi ya Visawe. East African Educational Publishers Ltd: Nairobi.
Mulokozi, M.M. (1996). Fasihi ya Kiswahili. Chuo Kikuu Huria cha Tanzania: Dar es Salaam.
Mulokozi, M.M.  (Mh.) (1999).  Tenzi Tatu za Kale. TUKI: Dar es Salaam.
Wamitila, K.W. (2003).  Kamusi ya Fasihi, Istilahi na Nadharia.  Focus Publications Ltd:  Nairobi.





“UCHAMBUZI WA UTENZI WA MWANAKUPONA: MAWAIDHA KATIKA TENDI.
UTANGULIZI.
Katika uchambuzi huu wa UTENZI WA MWANAKUPONA tunatarajia kuangalia vipengele kadhaa vya uchambuzi kama vile historia fupi ya mwandishi, vipengele vya  fani na maudhui, na vingine vitakavyojitokeza. Katika uchambuzi huu tutaonesha moja kwa moja nafasi ya mwanamke katika kumtunza mumewe. Hii ni kazi ya uchambuzi kwa hiyo itahusisha vipele mbalimbali vya uchambuzi. Kisha tutaonesha hitimisho na marejeo

HISTORIA FUPI YA MWANDISHI.
Mulokozi (1999) anatueleza kuwa Mwanakupona binti Mshamu Nabhany alizaliwa Pate mwaka 1810. Mwaka 1836 aliolewa na bwana Mohammed Is- Haq bin Mbarak. Lakini inasemekana kuwa alijulikana zaidi kwa jina la Mataka. Mwanakupona aliolewa na Bwanaa Mataka katika ndoa ya wake wengine watatu. Yasemekana kuwa Mataka alikuwa ni mtawala wa Siu na mpinzani mkubwa wa utawala wa waarabu huko Zanzibar. Mwanakupona alipata kuzaa watoto wawili na bwana Mataka ambao ni Mwana Hashimu bint Shee Mataka (1841-1933) na ndiye aliyetungiwa utenzi huu, na Mohammed bin Shee Mataka aliyezaliwa baina ya mwaka 1856 na 1858.
Tunendelea kuelezwa kuwa Shee Mataka alikuwa na watoto wengine watatu kwa wake wengine ambao ni Bakari alieyekufa vitani Pate mwaka 1855, Mohammed (mkubwa) ambaye ndiye aliyerithi utawala wa baba yake mwaka 1855 na kuendeleza upinzani uliokuwa umeanzishwa na baba yake dhidi ya utawala wa waarabu wa Zanzibar. Tunaelezwa kuwa baadaye Sayyid Majid, Sultan wa Unguja alimfanyia hila hadi alifanikiwa kumkamata na kumfungia katika Ngome ya Yesu, Mombasa ambako alifia huko mwaka 1868. Pia yasemekana kuwa baada ya kifo cha Mohammed (mkubwa) Omari alirithi utawala na kuishi hadi miaka ya mwanzo ya karne ya ishirini na alishiriki katika kupinga ukoloni wa Waingereza huko Kenya.
Pia yasemekana kuwa Mohammed (mkubwa) alikuwa mshairi na alitunga tungo za ILELE SIU ILELE na RISALA WA ZINJIBARI ambazo zilihusu mapambano yake na Sultani wa Unguja, na fitina za baadhi ya raia zake wa Siu. Baadaye tunaelezwa kuwa Mwanahashimu aliolewa mara mbili na kufanikiwa kupata watoto wawili ambao waliishi hukohuko Lamu. Alikuwa ni mshairi na alitunga mashairi kadhaa. Baadaye tunaelezwa kuwa kuna maafa yalimkuta bibie Mwanakupona na yaliisibu familia yake na hata aliiamua kuondoka Siu na kuhamia Lamu ambako ndiko alikotungia utenzi wake wa mwaka 1858. Inasemekana kuwa Mwanakupona aliuandika utenzi huu akiwa ni mgonjwa akisumbuliwa na maradhi ya tumbo la uzazi. Alihisi kuwa asingepona, hivyo akaamua kutunga utenzi huu ili uwe ni wosia kwa binti yake ambaye angebaki bila ya uongozi wa mama.
MUHTASARI WA UTENZI.
Kijamiii, Mwanakupona ni utenzi wa kimawaidha uliotungwa na Mwanakupona Binti Msham kwa ajili ya binti yake aliyeitwa Mwanahashimu bint Mataka mwaka 1858. Utenzi huu unaonakena kuwakilisha vyema tungo za utamaduni na maonyo ya wakati huo. Mtunzi aliutunga ili kumlenga binti yake aliyeitwa Mwana Hashimu kwa lengo la kumuonya lakini pia aligusia kwa vijana wengine wa kike wapate kuusoma utenzi huu ili nao wapate maonyo hayo (Ubeti wa 94 na 95). Utenzi huu unaonekana kuibadilisha jamii ya uswahilini baada ya kuona kuwa unafaa hasa kwa malezi ya kijadi hasa kwa watoto wa kike kwa kuwafunda. Yawezekana Jambo hili ndilo linaloufanya utenzi huu uonekane kuwa msaada wa jamii hata leo hii.
Kihistoria, tunaelezwa kuwa huu ni utenzi wa kale uliokuwa unaendana na mazingira ya wakati huo. Mwandishi aliuandika kwa kuilenga jamii ya wakati ule hasa kwa kufuata mila, desturi za jadi za wakati huo kama vile heshima ya ndoa, wanawake kuwekwa utawani, kutoonesha sura zao mbele ya watu, kumtukuza mume kama Mungu wao wa pili. Pia unaonekana kuwa ulikuwa ni utenzi wa kitabaka la utawala.
Kifasihi, UTENZI WA MWANAKUPONA ni utenzi pekee wa kishairi uliotungwa na mwanamke ambao unaonekana kuleta athari kwa waandishi wengine hata kuiga mfano wake wa kutunga tungo za kimawaidha kama vile Said Karama WASIA WA BABA, Shaaban Robert katika utenzi wa HATI NA ADILI, Zainab bint Humud, HOWANI MWANA HOWANI, UTENZI WA ADAMU NA HAWA.
FANI NA MAUDHUI.
FANI.
Senkoro (2011), anaeleza kuwa fani katika fasihi ni ule ufundi wa kisanaa anaotumia msanii katika kazi yake. Mpangilio wa vitushi, (episode) UTENZI WA MWANAKUPONA ni utenzi wenye jumla ya beti 102 ambao unaanza kwa mtunzi kumwita binti yake akaribie akiwa na wino na karatasi ili asikiilize wosia. Anasema kuwa yeye alikuwa ni mgonjwa hivyo hakupata muda wa kumpa wosia binti yake. Anamwambia binti yake kuwa aanze kwa kumtukuza Mungu wake na kumwomba rehema zake. Baada ya hapo anamwambia anataka kumpa hirizi ya kinga yake na kidani cha kujipambia. Halafu anaanza kumpa maonyo aliyokuwa ameyakusudia kama vile kuheshimu mume, kumheshimu mungu, kuwa mwaminifu, kuepuka umbeya, kushika dini na mengineyo. Hayo ni kuanzia ubeti wa (1-25).
Na kuanzia (ubeti. 26-36) mtunzi anaeleza namna mwanamke anavyotakiwa kumfanyia bwana yake. Miongoni mwa mambo hayo ni kutojibizana naye, kumpa kila anachokihitaji, kumuaga vizuri kila anapoondoka, kumpokea vizuri kila anapokuja, kumpapasa na kumpepea usiku, kumkanda mwili, kumsifia kwa watu wengine, kumwandalia chakula, kumnyoa ndevu, na kumpendezesha.
 Kuanzia (ubeti 37-56), mtunzi anaonesha namna mwanamke anavyopaswa kuwa yeye binafsi yaani mwanamke aliyeolewa inatakiwa awe msafi kimwili, avae vizuri na kujipamba kila siku, aombe ruhusu kwa mumewe kabla ya kutoka na akitoka asikawie kurudi na anapotembea asijifunue buibui lake na asiongee wala kunena na mtu yeyote njiani na aridhike kila anachopewa na mumewe.
Kuanzia (ubeti. 57-66) mtunzi anamwonya binti yake namna ya kuishi na watu wote kwa ujumla, yaani awe na upendo kwa watu wote bila kuangalia hadhi zao, afanye ushirikiano na wanandugu, marafiki na watu wengine pia awasaidie wanaohitaji msaada. Na atakapofanya hivyo malipo yake yatakuwa ni mbinguni.
Kuanzia (ubeti. 67-102) mtunzi anafanya dua ndefu ya kuwaombea watu wote wakiwemo watoto wake, anajiombea yeye mwenyewe, anawaombea waislamu kwa ujumla, na kisha anamalizia kwa kuwaombea wanawake wote wauosome utenzi huu ili wanufaike nao.
Hivyo tunaona kuwa japokuwa mtunzi amejitahidi kupangilia vitushi lakini inaonesha wazi kuwa amechanganya baadhi ya beti, yaani beti ambazo zilitakiwa ziwepo mwishoni amezipeleka kati ama mwanzoni mwa utenzi, na za mwanzoni kuzipeleka mwishoni ikiwa zingepaswa kuendana na beti fanani ili kukamilisha wazo. Kwa mfano beti za 92 na 93, zilipaswa kuwekwa mwanzoni maana zina mawazo ya mwanzoni kama vile maonyo kwa ujumla, ubeti 22 na 23 zingepaswa kuwekwa kati ya ubeti wa 11na 14 ili kusisitiza suala la dini, na ubeti wa 40 na 42 zingepaswa kuwekwa kati ya ubeti wa 36 na 37 ili kumwonya mtoto wa kike kuwa na tabia nzuri hasa kwa bwana yake kwa kuwa msafi na kufanya kazi.
Matumizi ya lugha, mwandishi huyu hajatumia sana lugha ya picha kama vile sitiari, tashibiha, tashihisi, methali nahau hata vitendawili na taswira japokuwa kwa kiasi fulani anaonekana kutumia lugha ya taswira kama vile hirizi, akionesha kuwa ni kinga ya kujikingia mtu aliyepatwa na matatizo ubeti ( 8-10), kidani,kama lulu au pambo (ubeti. 40) Anasema kuwa;
Na kidani na kifungo
Sitoe katika shingo
Muili siwate mengo
                                                          Kwa malashi na dalia
Hapa tunaona kuwa mwandishi ametumia taswira ya kidani inayomaanisha kuwa ni pambo au lulu inayovaliwa shingoni.
 Misamiati, aliyoitumia sio migumu sana inaeleweka japokuwa kwa kiasi kikubwa ametumia lahaja ya Kiamu na anaonekana kuimudu vyema lugha yake, lakini kwa mtu asiye mmilisi wa lahaja hiyo anaweza kupata mkanganyiko pindi anapousoma utenzi huu.
Muundo, kwa upande wa muundo mwandishi anaonekana kujitahidi kwa kiasi kikubwa kwani ametumia ushairi wa kufuata urari wa vina na mizani kwa kiasi kikubwa, na kila mshororo unaonekana kuwa na mizani 8.
Motifu, iliyojitokeza katika utenzi huu ni motifu ya msako wa peponi, yaani ile ya kumsaka Mwenyezi Mungu hasa kwa kutenda matendo mema, kutii maagizo yake pamoja na mwanamke kumheshimu mume. Mfano (Ubeti. 26-27) unasema;
26. Siku ufufuliwao
              Nadhari ni ya mumeo
     Taulizwa atakao
                                                               Ndilo takalotendewa
27.     Kipenda wende peponi
  Utakwenda dalhini
       Kinena wende motoni
                                                           Huna budi utatiwa
Beti hizi mbili zinatudhihirishia kuwa Mwanakupona aliona kuwa safari ya kufika peponi ni kubwa kwani kinachotakiwa ni kujipanga ili tuweze kuepuka adhabu ya jehanamu. Anamwambia mwanaye kuwa ili kushinda hilo ni vyema kumpenda mumewe na kumtii maana huko mbinguni Mungu atamuuliza kama alimpenda na kumtii huku duniani (Ubeti.28).
Keti naye kwa adabu
                                                        Usimtie ghadhabu
Akinena simjibu
                                                           Itahidi kunyamaa.
Ushujaa, wahusika wanaoelezwa katika utenzi huu sio mashujaa kama ilivyozoeleka katika tenzi zingine kama vile FUMO LIONGO, SUNDIATA, MAJIMAJI na zinginezo. Huu unaonekana kuwa ni utenzi wa kimawaidha ambao hauonyeshi ushujaa au unguli kwa sababu unatoa mawaidha mengi ya kijadi hasa kwa wanawake pamoja na binti yake. Hivyo tunaweza kusema kuwa utenzi huu haujasadifu ushujaa bali umekuwa na wahusika ambao ni binti yake anayeitwa Mwanahashimu, (ubeti .37), wanawake wengine (ubeti 94), Mungu ambaye anatajwa katika (ubeti. 5, 23, 36,72,73,82, 87 na 88) na mume (ubeti. 42, 47, 48).
Mianzo na miisho ya kifomula, mwandishi ameanza na sala au dua kama kawaida ya tendi za Kiswahili, katika sura ya kwanza (ubeti.4-7) anamwambia mwanaye aketi chini na Mungu wa rehema atasaidia katika kufanikisha jambo hilo. Mfano (ubeti.4) anasema;
Ukisa kutaqarabu
Bismillahi kutubu
Umsalie Habibu
Na sahabaze pamoya.
Pia anamalizia kwa shukrani ya kumshukuru Mungu kwa kumfanikishia shughuli nzima ya utunzi wa kazi yake na kuufanya usomwe na watu wengi ili uje kuwa nyenzo ya maisha yao. Mfano (ubeti.101-102)
101. Mola tutasahilia
Kwa Baraka za Nabia
Na masahaba pamoya
Dini waliotetea
102. Nahimidi kisalia
Kwa Tume wetu nabia
Ali zake na dhuria
Itwenee sote pia.
             MAUDHUI.
UTENZI WA MWANAKUPONA unaonekana kujadili masuala ya itikadi ya kijinsia yaani yakukubali na kuheshimu ngazi za mamlaka kama zilivyo bila kuzivunja kwa kuwa ni amri ya Mungu. Hata hivyo mawazo yake yanaonekana kuwa yalitokana na vyanzo kadhaa kama vile, mafundisho ya dini ya kiislamu, yanatokana na  mila na desturi za Waarabu zinazofuatwa na wenyeji wa pwani, mtazamo na ozoefu wa tabaka tawala la pwani. Mawazo yote haya yanaunganika na kutupa dhima kadhaa kama zifuatazo.
Dhima za utendi huu
Katika uchambuzi wa kazi yoyote ya kifasihi tunaona kwamba huwa na dhima mbalimbali ambazo huweza kuwa za kijamii, kihistoria na kiutamaduni. Lakini dhima hizo kwa kiasi kikubwa hutegemea muktadha na wakati wa utunzi wake. Kwa mfano utenzi huu ulikuwa na dhima zake nyingi kwa wakati ule lakini kwa sasa hauwezi kuwa na dhima ileile kwa kiwango chote kama ilivyokuwa wakati ule.
Kijamii, inaonyesha kuwa Mwanakupona aliuandika utenzi huu kwa kuzingatia tabaka lake na jamii yake. Kwani alikuwa katika jamii ya tabaka la Kifalme na hivyo dhima zake zilionekana kumsaidia zaidi binti aliyopo katika uwanja huo sio zaidi ya hapo. Kwa mfano alijaribu kuzungumzia masuala ya kutojichanganya na watumwa wakati wa kazi (ubeti. 20), kuepuka wajinga wasiojichunga (ubeti.21), kuwa mwaminifu na mpenda haki,(ubeti.14) kujinyenyekeza mbele za wakubwa, (ubeti. 15) kuepuka uropokaji (ubeti.19) kumheshimu Mungu na mtumewe (ubeti .23), kumheshimu mume (ubeti .31), kuheshimu wazazi, kuwa na upendo kwa wote (ubeti61-64), kuwa mtiifu (ubeti.13), kushika dini. Pia baadhi ya dhima hizo zinaonekana kuwa mwongozo kwa watoto wa kike mpaka kwenye jamii ya leo hii, na  labda ndio maana tunauona unafaa mpaka sasa. Pamoja na kugusia hayo hakujaribu kuzungumzia maswala ya tabaka la chini kama vile kulima, pamoja na maisha ya tabaka la chini kwa ujumla ila tu, anamwambia mwanaye awasaidie watu wasiojiweza mfano (ubeti.64) Anasema;
Na ayapo muhitaji
Mama kwako simuhuji
Kwa uwezalo mbuji
Agusa kumtendea
Hapa anadhihirisha wazi kabisa kuwa yeye anatoka katika tabaka la juu na kila kitu anacho.
Kihistoria, utenzi huu unatuonesha kuwa ni utenzi wa kale yaani wa miaka ya 1858 ambao ulitungwa na Mwanakupona kwa lengo la kumwonya binti yake na wanawake wengine. Ulikuwa na mashiko zaidi kwa wakati huo na kwa kiasi fulani mpaka sasa unaonekana kushika chati kwani unatoa maonyo na maadili kwa wanawake wa kisasa kama vile kuepuka umbeya, kuacha uvivu (ubeti .37), kuwa na adabu (ubeti.13),  kushika dini, upendo kwa wote, wanawake kuwaheshimu waume zao pamoja waume kuwaheshimu wake zao.
Kiutamaduni pia utenzi huu unaoneka kuwa kwa kiasi kikubwa unazungumzia mambo ya kitamaduni hasa utamaduni wa kufuata mila, desturi na jadi za Waswahili, na kwa kiasi kidogo unagusia pia tamaduni za Kiarabu. Kwa upande wa Waafrika kama tunavyojua kuwa wao wana mila na desturi zao za kijadi ambazo hutokea baada ya kijana kuonekana anafikia hatua ya makuzi. Hivyo jamii huchukua jukumu la kuwafunda vijana wa kike na kiume. Kwa mfano hufundwa kuhusu mambo ya ndoa (namna ya kuishi na mume) na maisha kwa ujumla. Hata ndani ya utenzi huu tunaona hayo yakifanywa na mtunzi kwa binti yake, akimwonya juu ya mambo kadhaa ya kiutamaduni kama vile; adabu na heshima, kuepuka umbeya, kuepuka fitina, kuepuka uchoyo (ubeti.64), kuepuka uvivu (ubeti .37), kuwa msafi na kujipamba ili kufurahisha na kumvutia mume ubeti. (40-42), kutomnyima mume chochote anachokitaka (ubeti.29) na kumhudumia kitandani mfano. (ubeti.31) anasema.
Kilala siikukuse
Mwegeme umpapase
Na upepo asikose
Mtu wa kumpepea.
Funzo hili liko katika mila za ndoa kwani utamaduni wa Waswahili husisitiza sana masuala kama hayo hasa kwa kudumisha ndoa kwa kupendana na kutimiziana mahitaji mbalimbali ili kuishi kwa furaha na amani ndani ya nyumba mfano kutabasamu kwa mke kila anapomwona mume wake (ubeti.50).
Pia utamaduni wa Kiarabu  ulioguswa ni kama vile; namna ya mwanamke anapovaa na kutoka nje ya nyumba yake inatakiwa aweje, mwandishi anatuonyesha kuwa Waarabu wanatamaduni zao ambazo wanazifuata na kuzitekeleza lakini kwa sasa zinaonekana kabisa kuingia katika utamduni wa waswahili na tunazifuata. Kwa mfano masuala ya kutawishwa kwa mwanamke pamoja na mavazi (ubeti 44-45), pia mwanamke anaambiwa kuwa anapotoka asiangalie wala kuongea na watu njiani, (ubeti .46) anasema
Wala sinene ndiani
Sifunue shiraani
Mato angalia tini
Na uso utie haya.
Tunaona kuwa hizi ni mila za kiarabu ambazo kwa sasa zinaonekana kuleta athari mpaka kwetu mpaka sasa.
Suala la dini, sehemu kubwa ya UTENZI WA MWANAKUPONA unaonekana kujadili zaidi kuhusu maudhui ya kidini na kusisitiza haja ya kuzingatia mafunzo ya dini ya kiislamu. Kama vile, kumtii Mungu na mtume wake (ubeti.23), kupenda na kutenda haki kama dini inavyotaka (ubeti. 12), kumtii mume na kuishi naye kwa upendo kama dini inavyotaka. (Ubeti.26-27), pia utenzi huu unatufundisha kuwa Mungu pekee ndiye anayeweza kutenda chochote unachohitaji na kama ni hivyo basi hatuna budi ya kutanguliza maombezi yetu kwake popote tunapofanya jambo fulani hata baada ya kumaliza shughuli yoyote ni vyema pia kumshukuru. Mfano huu tunauona pia kwa Mwanakupona mwenyewe ambaye alianza kwa dua na kumalizia tena na dua ubeti. (4-7, 66-102).
Falsafa ya mwandishi juu ya utenzi huu inaonekana kuwa mwanamke hawezi kufika mbinguni kama hajamtendea mume wake mambo anayopaswa kufanyiwa katika maisha ya ndoa.
Hivyo tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa UTENZI WA MWANAKUPONA unaonekana kuwa nguzo ya mafunzo na maonyo kwa wanawake hata wa kizazi cha sasa lakini kwa kuangalia kwa baadhi ya mafunzo ambayo yanaendana na wakati huu maana mafunzo mengi yaliyoelezwa ni ya wakati wa zamani na hayana maana kwa wakati huu. Pia utenzi huu unaonekana kumdidimiza sana mwanamke hata kutopewa uhuru wa kuweza kufanya mambo mengine ya kimaendeleo kwani unamfanya mwanamke muda wote awaze namna ya kumriwaza mume tu.
MAREJEO
Mulokozi, M.M. (1999) Tenzi Tatu za Kale. Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili: Dar es Salaam.
Senkoro, F.E.M.K (2011) Fasihi. Dar es salaam. KAUTTU.

  


Uchambuzi wa makala ya mwandishi Jan Vansina. Hapo Zamani za kale: Mapokeo Simulizikama historia ya Afrika
MUHTASARI WA MAKALA
Mwandishi anaanza kwa kumnukuu Mbope Luis wa Kongo anayesema “ vitabu vyetu vipo kichwani mwetu”.
Makala imejaribu kuelezea historia ya masimulizi jadi yaliyokuwa yanapatikana Afrika. Mwandishi aanatofautisha jadi za namna mbili kwa kutumia jamii za Kiafrika na za Ulaya. Anasema kuwa tofauti na Ulaya ambako kusoma na kuandika vilikuwa kama kielelezo cha ustaarabu, jamii za Kiafrika kabla ya kuja ukoloni zilijitosheleza na kujieleza kwa kutumia mapokeo simulizi. Mwandishi anasisitiza kuwa nafasi na dhima ya mapokeo simulizi barani Afrika iliendelea kustawi hata baada ya kuingia kwa ustaarabu wa kusoma na kuandika, kwa maneno mengine Vansina anakiri kuwa kuna  uhusiano mkubwa kati ya jadi ya mapokeo simulizi na jadi ya maandishi.  Katika kulithibitisha hili anamtumia Profesa Willam A. Brown ambaye aliikuta barua huko masino ( Mali ) ambayo maudhui yake yalielezwa kwa kurejelea mambo mbalimbali. Yaliyokuwa yamesahaulika lakini yalikumbukwa kutokana na barua hiyo, barua hiyo ilikuwa kama chombo cha kutunza kumbukumbu hizo ili kurithisha desturi hizo.
Muundo, mfumo na dhima ya mapokeo simulizi ya jamii hubadilika kutokana na  maingiliano yanayotokea katika jamii ambayo husababishwa na mabadiliko ya kuachwa kwa vitu muhimu katika wakati maalum na hatua za mabadiliko hayo huitwa muundo wa usahaulifu “structural amnesia” kwa kuwa masimulizi jadi ya jamii, utamaduni ulirithishwa kwa mawasiliano ya ana kwa ana na kubadilisha maudhui, kila jamii ilieleza; imani, maadili, mawazo na mtazamo wake katika fasihi.
Levis Straus anazungumzia muundo ndani wa mazungumzo, anasema kila kinachozungumzwa kina muundo kama huo, ila hujidhihirisha zaidi katika masimulizi. Muundo huu unahusisha msukumo, mtiririko wa maonesho, kujenga kilele kimoja au zaidi, usambamba, uradidi na kubadilika kwa onesho na hivi vyote lazima vichanganuliwe kabla.
Pia anasema athari yake katika maudhui yanaweza kuonekana na mtu yeyote anayechanganua maana ya ishara “ taswira za tendi” au taswira maarufu katika historia.
Katika nukuu ya Levis Straus na wanaantropolojia waliofuata walisema masimulizi mengi yalikuwa ya kitalii.
Kila tarihi ilieleza muundo halisi wa ishara za msingi zinazoeleza sio vitu vyenye thamani tu vilipendwa na jamii ya watu kiundani lakini pia utendaji wa kifikra wa binadamu, fikra za mwanadamu hazina budi  kuwa na ushirikiano wa kifikra kabla ya kuelewa na kuwasiliana.
KUSUDI LA MWANDISHI
Kusudi la mwandishi katika kuandika makala hii ni kutaka kuthibitisha kuwa Afrika kulikuwa hakuna masimulizi, mfano ngano, tendi, misemo, hadithi (masimulizi).
NAMNA ALIVYOPANGA KUSHUGHULIKIA
Alishughulikia suala hili kwa kupitia tafiti za wataalamu wengine ambao tayari walikuwa wameshafanya utafiti  kuhusu mapokeo simulizi, mfano alimtumia Ernest Bernheim, ambaye katika utafiti wake alidondoa nyimbo, ngano, na saga, hekaya, masimulizi mafupi, misemo na methali.
Pia alimtumia Profesa William A. Brown kwa kutumia barua yake ambayo aliikuta huko Masino ( Mali) iliyokuwa na maudhui mengi kuhusu Afrika.
Baada ya hapo aliamua kufanya tafiti yeye mwenyewe ili aweze kuziba pengo la wale wataalamu wengine na kuweza kulinganisha kile walichokipata wataalamu waliopita na kile alichokipata yeye kuhusu mapokeo simulizi ya Kiafrika.
JINSI ALIVYOPATA DATA
Aliangalia masimulizi ya Warundi na Warwanda na kuona kuwa masimulizi ya waburundi yalikuwa mafupi kwa sababu yanatolewa katika mkusanyiko usiokuwa rasmi lakini masimulizi ya Warwanda yalikuwa katika mchanganyiko yaani marefu na mafupi.
Pia waliangalia nyaraka zilizoandikwa, makumbusho sanaa halisi, malighafi ya tamaduni na habari ya Wanaismu. Japokuwa data zote hizi isipokuwa ile ya matini iliyoandikwa na zilikuwa zimesomwa na wataalamu wengine.
Zilizoandikwa katika Afrika zilifanywa na wageni ambao hawakuelewa shughuli za jamii na tamaduni walizoshughulikia. Aligundua kuwa nyaraka za zamani zilikuwa na ukweli zaidi, mfano kwa kutumia barua aliyoikuta Masino ( Mali ) na kwa kuangalia masimulizi ya Warwanda na Waburundi.
DATA HIZO ZILIKUWAJE?
Jan Vansina anasema jamii nyingi za Afrika Kusini mwa jangwa la sahara zilitumia mapokeo simulizi kwa muda mrefu, japokuwa zilitumia maandishi kwa kiasi kidogo, hivyo zilitawaliwa na jadi ya kimasimulizi. Kila kitu kilichohusu maisha yao, ikiwemo historia yao kilihifadhiwa katika masimulizi hayo. Hivyo mwanahistoria yeyote mwenye nia ya kutaka kuifahamu historia ya Wafrika hana budi kutambua kuwa mhimili mkuu wa historia ya jamii hiyo ni mapokeo simulizi.
Kwa upande wa Tanzania maeneo mengi ya kati, mapokeo simulizi yalikuwa chanzo kikuu cha historian a maarifa mpaka miaka ya 1880, ambapo historia ya falme za Kongo zilikuwa zimebadilishwa kuwa katika maandishi.
Hayo mapokeo simulizi yalitumika katika siasa ya kijamii, kiuchumi, dini, misafara mbalimbali na shughuli za kiutamaduni.
Data hizo pia zilionyesha mwingiliano wa matini katika mapokeo simulizi, kuhusu hili Vansina anasema suala la mwingiliano matini huhusisha ujitokezaji wa vipengele vya nyimbo za kidini, methali, ngano, katika mapokeo simulizi kama masimulizi ya kijadi yaliwekwa katika mpangilio ( tarihi za matukio mbalimbali ).
Kwa upande mwingine Vansina anafafanua kuwa nyimbo maarufu katika baadhi ya jamii ziliimbwa kwa kurudiwa mara nyingi na zingine kwa nadra. Kwa mfano katika familia za kifalme miongoni mwa jamii za Bushoong ya Kasai (Kongo) nyimbo hizo ziliimbwa kipindi cha kumsimika mfalme. Huko Afrika Magharibi miongoni mwa jamii ya Wadogoni nyimbo hizo ziliimbwa katika shughuli za kidini na kijamii kama vile matambiko na sherehe za kijadi. Katika jamii hii, nyimbo mashuhuri zilizohusu matambiko na sherehe za kijadi zilisimuliwa kwa jamii nzima  hasa mara moja kila baada ya miaka sita.


HITIMISHO LAKE
Kutokana na utafiti wake alioufanya kwa kutumia data mbalimbali, alihitimisha kwa kusema kuwa Afrika kuna jadi ambazo zimetokana na masimulizi.
UFAWAFU WA MAKALA
Kila jamii ina umuhimu wake hata kama inatimiza kwa kiasi kidogo mambo mazuri au malengo au dhima yake inaweza kubadilika kipindi cha urithishwaji kwa sababu jamii imebadilika, tathmini ya kuharibika ambayo hutokana na msukumo katika jamii wakati mwingine ni vigumu kukadiria.
Kuna uhusiano mkubwa kati ya mapokeo simulizi na maandishi, katika kuthibitisha hili anamtumia Profesa William A. Brown aliyeikuta barua Masino ( Mali ) ambayo maudhui yake yalielezwa kwa kurejelea mambo mbalimbali yaliyosababishwa lakini yalikumbukwa kutokana na barua hiyo.
Jadi nyingi za Kiafrika ni za kimasimulizi zikifungamana na nyimbo na mashairi lakini haziangukii katika aina ya jadi za Ulaya. Pia kimuundo zipo kama masimulizi, ndefu kuliko zilivyo hadithi zingine.
Maelezo hayo yana mchango mkubwa kwani yanadhihirisha kuwa Afrika kulikuwa na tendi ambazo zilikuwa katika umbo la masimulizi na kishairi.
MAPENDEKEZO
Mwandishi alipokuwa akisema jadi zimetokana na masimulizi hususani ushairi. Je huo ushairi ulikuaje? (ushairi ulikuwa unafuata kanuni au lah!) kwa hiyo utafiti ufanyike zaidi ili kujua huu ushairi ulikuaje.
Kama hizo jadi zilikuwa katika usimulizi, usimulizi huo ulikuwa ni rasmi au sio rasmi? Tunapendekeza mwandishi afafanue kuwa jadi zimetokana na usimulizi gani haswa, kwa hiyo tafiti ziendelee kufanyika.
HOJA NZITO
1. Uasili wa kijadi unaweza kuwa wa namna mbalimbali, kwanza kwa kushuhudia matukio, pia kutoka katika maandishi, mfano ngano ubunifu wa matukio ya kihistoria au shughuli za kifasihi, visa vya kubuni pamoja na vya kuiba.
2. Afrika kuna tendi ambazo zimetokana na masimulizi ya kijadi.
3. kuna uhusiano mkubwa kati ya masimulizi jadi na maandishi.
4. Nyaraka zilizoandikwa katika Afrika zilifanywa na wageni ambao hawakuelewa shughuli za jamii na tamaduni waliyoshughulikia.
5. kila jadi ina umuhimu wake hata kama itatimiza kwa kiasi kidogo mambo mazuri au maadili.
6. muingiliano matini katika masimulizi jadi ni jambo ambalo haliepukiki mfano; nyimbo za kidini, methali, ngano, yaliwekwa katika mpangilio (tarihi ) za matukio.
HOJA TETE
Jadi za ulaya zina muundo rahisi lakini zina mpaka rasmi na ni za kawaida katika ubora.

JAMBO MUHIMU KATIKA MAPOKEO SIMULIZI YA KIFRIKA
Mapokeo simulizi yamekuwa yakitumika na yanatumika zaidi na zaidi katika historia ya Afrika. Mtiririko huu ni ushahidi katika makala za kihistoria za Kiafrika. Tangu mwanzo mwa mwaka 1960 makala zilikuwa na angalau kipengele kimoja kwa mwaka kilichokuwa kikizungumzia mapokeo simulizi, katika vipindi vyote vitatu vya karibuni vya historia ya Afrika Mashariki vimekuwa vikielezea Mapokeo simulizi kati  ya mwaka 1500-1850, hasa sehemu za kati ya Tanzania.
Utaratibu wa kukusanya mapokeo simulizi unapatikana kwa kufuata utaratibu wa kutafuta tamaduni za kifamilia  au hata kwa kuona, kuhesabu matukioa kutoka kipindi kimoja hadi kingine. Kwa mfano, katika kipindi cha  ukoloni tukio kama vile vita vya majimaji (1905-1907) Afrika Mashariki. Hali kama hii pia ilipatikana huko Afrika ya kati na maeneo ya Sudan.Jitihada za kukusanya na kuhifadhi data za kimapokeo simulizi zinadhihirika pia huko Jamhuri ya Niger ambapo tunafahamishwa kuwa kuliandaliwa eneo maalumu kwa ukusanyaji na utunzaji wa sanaa jadiyya. Swali ambalo mwandishi anajiuliza ni kuwa pamoja na kuwepo kwa jitihada za kutosha katika kukusanya na kuhifadhi data za mapokeo simulizi hakuna haja ya kujiuliza maswali kuwa Mapokeo simuliz yanaweza kutumika kama chanzo cha taarifa za kihistoria?.  Anaendeleza mjadala kwa kusema kuwa haja ya kujiuliza ipo kwani suala hili  linategemea namna ya ukusanyaji na uchanganuzi wa data.

No comments:

Post a Comment