Tuesday 22 January 2013

JE? WAJUA KUWA FONETIKI NI MOYO WA FANOLOJIA?


Fonetiki na Fonoloji.
Fasili ya taaluma ya fonolojia haiwezi kukamilika, na pengine kueleweka iwapo hakuna linalosemwa kuhusuiana na taaluma ya fonetiki. Hali hii inatokana na ukweli kuwa kuna uhusiano wa kinasaba kati ya fonolojia na fonetiki. Massamba na wenzake (2004:5) wanaeleza ukweli huu kwamba:
Fonetiki na fonolojia ni matawi mawili tofauti ya isimu lakini yenye kuhusiana sana. Uhusiano wa matawi haya unatokana na ukweli kwamba yote mawiliyanajihusisha na uchunguzi na uchambuzi unaohusu sauti za lugha za binadamu.
Kutokana na ukweli huu, jitihada za kufasili dhana ya fonolojia inaelekea kuwa nyepesi, dhana hizi mbili zinapofasiliwa kwa mlinganyo. Tuanze na fonetiki.
Fonetikini Nini?
Fonetiki ni tawi la isimu linalochunguza sauti za kutamkwa na binadamu ambazo huweza kutumika katika lugha asilia. Massamba na wenzake (kama hapo juu) wanafasili fonetiki kuwa ni tawi la isimu linalohusika na uchunguzi na uchambuzi wa taratibu za utoaji, utamkaji, usafirishaji, usikilizaji na ufasili wa sauti za lugha za binadamu kwa ujumla. Wanasisitiza kwamba, kinachochunguzwa katika fonetiki ni (maumbo mbalimbali ya sauti zinazoweza kutolewa na alasauti za binadamu (yaani sauti za binadamu zinazotamkwa tu). Kipashio cha msingi cha uchambuzi wa kifonetiki ni foni.
Foni ni sauti yoyote inayotamkwa na binadamu na inayoweza kutumika katika lugha fulani. Hivyo basi, foni ni nyingi sana na hazina maana yoyote. Wanafonetiki hudai kuwa foni zimo katika bohari la sauti (dhana dhahania) ambalo kila lugha huchota sauti chache tu ambazo hutumika katika lugha mahususi. Sauti chache zinazoteuliwa na lugha mahususi kutoka katika bohari la sauti huitwa fonimu.
Matawi ya Fonetiki: Kuna mitazamo miwili tofauti kuhusiana na matawi ya fonetiki. Mtazamo wa  kwanza ni ule unaodai kuwepo matawi matatu; na mtazamo wa pili ni ule niunaodai kuwepo matawi manne. Mtazamo wa kuwepo matawi matatu unataja fonetiki matamshi, fonetiki akustika, nafonetiki masikizi. Mtazamo wa kuwepo matawi manne. (kama Massamba na wenzake ( kama hapo juu), pamoja na matawi tuliyokwisha yataja, wanaongeza tawi fonetiki tibamatamshi.
Fonetiki mahuchunguza jinsi sauti za lugha zinavyotamkwa kwa kutumia alasauti. Hususani, huchunguza namna na mahali pa kutamkia sauti husika. Fonetiki akustika huchunguza jinsi mawimbi ya sauti yanavyosafiri kutoka katika kinywa cha mtamkaji hadi kufika katika sikio la msikilizaji. Fonetiki masikizi hujihusisha na mchakato wa ufasili wa sauti za lugha, hususani uhusiano uliopo baina ya neva za sikio na za ubongo. Na fonetiki tibamatamshi ni tawi jipya lililozuka mwanzoni mwa karne hii, ambalo huchunguza matatizo ya utamkaji ambayo binadamu huweza kuzaliwa nayo au kuyapata baada ya kuzaliwa. Ni tawi linalojaribu kutumia mbinu za kitabibu kuchunguza matatizo na namna ya kuyatatua.
Fonolojia ni Nini?
Fonolojia ni taaluma ya isimu inayochunguza mifumo ya sauti za kutamkwa zinazotumika katika lugha asilia mahususi za binadamu. Inapolinganishwa na fonetiki, inasisitizwa kuwa fonolojia ni tawi la isimu linalochunguza mifumo ya sauti za lugha mahususi tu, kama vile sauti za kiswahili, Kiingereza, Kikongo, n.k. Hata hivyo, wapo wanaisimu wanaoelekea kukubaliana kuwa kuna fonetiki ya lugha mahususi pia, na kuna fonolojia ya jumla, na fonetiki ya lugha mahususi. Mathalani, Massamba (1996) licha ya kufasili kuwa fonolojia  ni taaluma ya isimu inayochunguza mfumo wa sauti za lugha mahususi, anaenda mbele zaidi na kudai kuwa fonolojia inaweza kuchunguza sauti kwa ujumla wake bila kuzihusisha na lugha mahususi.
Akmajian na wenzake (2001), nao wanadokeza msimamo kama wa massamba wanapodai kwamba fonolojia inaweza kuchunguzwa kwa mitazamo miwili tofauti. kwanza, fonolojia kama tawi dogo la isimu linalochunguza mfumo na ruwaza za sauti za lugh mahususi ya binadamu; pili fonolojia kama sehemu ya nadharia ya jumla ya lugha ya binadamu inayohusika na tabia za jumla za mfumo wa sauti za lugha asili za binadamu. Katika mhadhara huu, hata hivyo tutakuwa wafuasi wa mtazamo unaoona kuwa fonolojia ni tawi la isimu linaloshughulikia mfumo wa sauti za lugha mahususi, hivyo tuna kwa mfano, fonolojia ya Kiswahili, fonolojia ya Kiingereza, fonolojia ya Kiha, fonolojia ya Kihehe, na fonolojia ya Kibena. Kipashio cha msingi cha fonolojia ni fonimu.
Fonimu.
Ni kipashio kidogo kabisa cha kifonolojia kinachoweza kubadili maana ya neno. Hivyo basi, fonimu ina maana, kwa kuwa inaweza kubadili maana ya neno inapobadilishwa nafasi katika neno husika. Foni chache zilizoteuliwa kutoka katika bohari la sauti ili zitumike kwenye mfumo wa sauti za lugha mahususi ndiyo fonimu. Hivyo, fonimu ni chache ikilinganishwa na foni. Idadi ya fonimu za lugha hutofautiana kati ya lugha moja na nyingine. Mathalani, Kiarabu kina fonimu ishirini na nane (28), Kiswahili kina fonimu thelathini (30), Kifaransa kina fonimu thelathini na tatu (33) na Kiingereza kina fonimu arobaini na nne (44). Sauti ambayo huweza kubadilishwa nafasi yake katika neno lakini maana ikabaki ileile huitwa alofoni.
Alofoni ni kishio cha kifonolojia kinachotaja hali ambapo fonimu moja hutamkwa na kuandikwa tofautitofauti bila kubadili maana ya neno. Mfano:
·         Fedha na feza
·         Sasa na thatha
·         Heri na kheri
Kwa kifupi, alofoni ni matamshi tofautitofauti ya fonimu [sauti] moja.
Mitazamo juu ya Dhana ya Fonimu.
Juhudi za kufasili dhana ya fonimu zilizofanywa na wanaisimu mbalimbali zimezua mitazamo mbalimbali ya namna ya kuchambua dhana hii. Hadi sasa, mitazamo mitatu ifuatayo ndiyo hujulikana zaidi.
(i)                 Fonimu ni tukio la Kisaikolojia.
Huu ni mtazamo uliokuzwa na kutetewa na wanasarufi geuzi-zalishi, mwanzilishi wake akiwa ni Noam Chomsky. Kwa mujibu wa mtazamo huu, fonimu ni dhana iliyo katika akili ya mzungumzaji wa lugha. Mtazamo huu unadai kuwa kila mzungumzaji wa lugha ana maarifa bubu ya idadi na jinsi ya kutamka fonimu za lugha yake Chomsky anayaita maarifa haya kuwa ni umilisi (competence). Anadai kuwa maarifa haya ya fonimu hufanana kwa kiasi kikubwa miongoni mwa wazungumzaji wa lugha moja husika. Kinachotofautiana ni jinsi ya kudhihirisha (kutamka) fonimu hizo, yaani utendi (performance). Chomsky anabainisha kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuhitilafiana baina ya umilisi na utendi kutokana na matatizo mbalimbali ambayo mzungumzaji hukabiliana nayo. Matatizo hayo ni kama vile uchovu, ulemavu wa viungo vya matamshi (alasauti za lugha), athari za mazingira, ulevi na maradhi. Hivyo kutoka na hali hii, fonimu hubaki kuwa tukio la kiakili, yaani kisaikolojia tu.
(ii)               Fonetikinitukio la Kifonetiki.
Wafuasi wa mtazamo huu wanaongozwa na Daniel James. Ambaye anaiona fonimu kuwa ni {umbo} halisi linalojibainisha kwa sifa zake bainifu. Anadai kuwa fonimu huwakilisha umbo halisi la kifonetiki na inapotokea kukawa na fungu la sauti katika fonimu moja, sauti hizo huwa na sifa muhimu za kifonetiki zinazofanana. Hivyo, fonimu ya Kiswahili ni kitita cha sauti za msingi pamoja na alofoni zake.
(iii)             Fonimu ni Fonolojia.
Huu ni mtazamo wa kidhanifu, ambapo huaminika kuwa fonimu ni kipashio cha kimfumo, yaani fonimu huwa na maana pale tuinapokuwa katika mfumo mahususi. Mwanzilishi wa mtazamo huu ni Nikolai Trubetzkoy. Yeye huamini kuwa fonimu ni dhana ya kiuamilifu na uamilifu huu hujitokeza tu fonimu husika inapokuwa katika mfumo wa sauti wa lugha husika. Kwa mujibu wa mtazamo huu, fonimu ni kipashio kinachobainisha maana ya neno. Mtazamo huu hutumia jozi sahihi kudhihirisha dai lake. Mathalani, maneno baba na bata yana maana tofauti kwa sababu ya tofauti ya fonimu /b/ na /t/. Mtazamo huu hujulikana kuwa ni wa kifonolojia. Na kwa hakika, mawazo haya ndiyo yaliyoshika mzizi zaidi katika taaluma ya fonolojia na ndiyo inayofunzwa hivi sasa katika sehemu nyingi ulimwenguni.
UhusianokatiyaFonetikinaFonolojia
FONETIKI
FONOLOJIA
HuchungasautizakutamkwanaBinadamu
HuchunguzasautizakutamkwanaBinadamu
Ni pana {huchunguzasautinyingi}
Ni finyu {huchunguzasautichachetu}
Ni kongwe.
Ni changa.
Huchunguzasautipekepeke
Huchunguzasautikatikamfumo.
Huchunguzasautikwaujumla
Huchunguzasautizalughamahususi, kama Kiswahili, naKinyeramba.
Kipashio cha msinginifoni
Kipashio cha msinginifonimu.

UhusianokatiyaFoninaFonimu.
FONI
FONIMU
Hazimamaana
Zinamaana
Zipopekepeke
Zimokatikamfumo
Nyingi
Chache

Huwezakujitokezakamaalofoni
Zinaponukuliwa, alamayamabano, “{ }” hutumika
Zinaponukuliwa, alamayamabanomshazari, “/ /” hutumika




12 comments:

  1. kaka vipi? napenda kuandika makala ya kiswahili kuhusu umuhimu wa fasihi katika maisha ya kila siku. je nifanyaje??

    ReplyDelete
    Replies
    1. jambo la msingi kwanza fanya utafiti kuhusu kile unachotaka kuandikia, kinaweza kuwa kimekugusa wewe moja kwa moja au mwenzako ali mladi uwe na uwezo wa kupangilia mawazo na mwisho utafanikiwawazo hongera kwa kuwa na moyo wa KUKIPENDA KISWAHILI KWANI NDIYO LUGHA MAMA KWETU.

      Delete
  2. kaka mi naomba unisaidie utata unaojitokeza wakati wa uandikaji irabu za kifonetiki

    ReplyDelete
  3. utata upo wapi yani kwa sababu unaposema irabu za kifonetiki ni zile ambazo hazihusiani na lugha yoyote ile na nafikiri zipo 20

    ReplyDelete
  4. asante kwa kuitukuza lugha yetu ya kiswahili.....................!!

    ReplyDelete
  5. Je nisaidie kuelewa iwapo ujuzi wa fonetiki ni muhimu katika usomi wa kiswahili

    ReplyDelete
  6. Mimi naomba hoja tano za mfanano na uhusiano kati ya fonetiki na fonolojia.

    ReplyDelete
  7. Naomba kujua uhusiano baina ya fonetiki na fonolojia🔰

    ReplyDelete
  8. Utata kwa uhusiano baina ya fonolojia na fonetiki....vile umeeleza pale juu ni utofauti au ubusiano? Naomba kujua

    ReplyDelete
  9. Kazi nzuri isipokuwa hujaambatanisha marejeo

    ReplyDelete
  10. Merkur & Ferencia: Merkur & Ferencia Merkur
    Merkur & Ferencia merkur - Merkur & Ferencia Merkur in Solingen, febcasino Germany - Merkur - 1xbet 먹튀 Merkur https://febcasino.com/review/merit-casino/ Merkur - MERKUR - Merkur & Ferencia Merkur apr casino

    ReplyDelete